

Lugha Nyingine
深圳罗湖规模最大科技企业孵化器获授牌
Baraza la chini la Bunge la Rwanda limepitisha kwa kauli moja jana Jumanne sheria inayoidhinisha makubaliano ya amani na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ikilenga kurejesha amani na usalama katika Eneo la Maziwa Makuu.
Makubaliano hayo yaliyosainiwa tarehe 27 Juni mjini Washington, D.C. na kuungwa mkono na wabunge wote 76 waliopo, yanalenga kutafuta ufumbuzi wa mivutano na changamoto za kiusalama za muda mrefu kati ya nchi hizo mbili.
Kwenye mjadala wa bunge kuhusu makubaliano hayo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Rwanda Olivier Nduhungirehe amesema, makubaliano hayo yalisainiwa nchini Marekani, ambayo ilishiriki katika mchakato huo, chini ya upatanishi wa Qatar na uungaji mkono wa Umoja wa Afrika.
“Hii ni hatua muhimu kuelekea kurejesha amani, usalama na kuaminiana kati ya Rwanda na DRC” Nduhungirehe amewaambia wabunge.
Mandhari ya Kipekee ya Karst katika Mkoa wa Guizhou yavutia watalii
Tamasha la kimataifa la densi lafunguliwa katika Mkoa wa Xinjiang, China likiwa na maonyesho 52
Wakulima wa China wawa na pilikapilika za uzalishaji wa kilimo katika kipindi cha Dashu
Maliasili nyingi za chumvi zaongeza mapato ya wanakijiji katika Wilaya ya Gegye, Xizang, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma